The United Republic of Tanzania
The Office of the Attorney General

“SISI OFISI YA MWANASHERIA MKU...

“SISI OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI TUNAAMINI NYINYI WAHARIRI NI ASKARI WA KALAMU” - NAIBU MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Samwel M. Maneno amesema kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ina amini kuwa Wahariri wa Vyombo vya Habari ni Askari wa Kalamu kwakuwa wanauwezo wa kuelimisha, kulinda na kusimamia masuala mbalimbali yanayogusa Jamii ikiwemo misingi ya Sheria na Utawala Bora.

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wahariri wa Vyombo vya Habari nchini tarehe 11 Septemba, 2025 Jijini Dodoma.

Akizungumza katika ufunguzi wa kikao hicho Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameeleza kuwa Serikali inatambua mchango mkubwa wa Vyombo vya Habari katika kujenga Utawala Bora na Uwazi ambapo amesema kuwa Vyombo vya Habari ni daraja muhimu la kuunganisha Serikali na wananchi, na ndio maana ni muhimu sana kwa wahariri kuwa na uelewa wa kutosha wa masuala ya kisheria ili waweze kuripoti kwa usahihi na bila upotoshaji.

“Sisi Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali tunaamini nyinyi Wahariri wa Vyombo vya Habari ni Askari wa Kalamu kama tulivyo sisi Mawakili wa Serikali, kwakua mna jukumu muhimu la kulinda na kusimamia misingi ya Utawala Bora kwa kutoa taarifa sahihi kwa wananchi.” Amesema Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Katika hatua nyingine, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesema kupitia kikao hicho Wahariri watapata uelewa wa kutosha wa m