HABARI PICHA
Imewekwa:
13 Nov, 2025
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari akiwasilisha Azimio la Bunge la kumthibitisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bungeni Jijini Dodoma, tarehe 13 Novemba, 2025.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali amewasilisha Azimio hilo mbele ya Bunge kufuatia uteuzi uliofanywa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kumteua Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

