WATUMISHI 80 WA OMMS WAPATIWA KOMPYUTA MPAKATO

Imewekwa: 26 May, 2023
WATUMISHI 80 WA OMMS WAPATIWA  KOMPYUTA MPAKATO

WATUMISHI 80 OMMS  WAPATIWA  KOMPYUTA MPAKATO

Na  Mwandishi wetu

 

MTUMBA-Menejimenti ya  Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  katika kikao chake  kilichoketi  chini ya Uenyekiti wa Naibu  Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Dkt. Evaristo Longopa  kimepitisha mgao wa  Kompyuta  Mpakato  kwa  watumishi  80

Kikao hicho  kimefanyika leo (Ijumaa) katika ukumbi wa  Mikutano  Mtumba  ambapo kabla  mgawanyo huo  Mwenyekiti   alitoa  maelezo  mafupi yakiwamo ya  namna  vifaa hivyo vya TEHAMA vilivyopatikana na  mgawayo wake ambao  umezingatia  masuala  kadhaa.

“Ndugu wajumbe tumekutana leo katika kikao hiki  kama menejimenti ili  tuweze kujadiliana  na kupitisha mgao wa komputa mpakato ambazo  kati  yake  ni zile ambazo  Ofisi  ilikabidhiwa na Mhe. Rais na nyingine zinatokana na  Mradi wa BSAAT”. Akaeleza Mwenyekiti

Akaeleza  kwamba, mchanganuo wa ugawaji   vifaa hivyo  umezingatia  mambo kadhaa   ambayo ni   Tange la Watumishi wa Ofisi,  mahitaji  kutokana na  majukumu ya kila siku ya watumishi husika na waajiriwa wapya  hasa mawakili wa Serikali .

Dkt  Longopa akaeleza Zaidi kwamba,  watumishi ambao hawapo kwenye mgao huu na pia hawana vifaa hivyo vya TEHAMA  pamoja na   baadhi ya  Vitengo   watapewa kipaumbele katika mgao  utakaofuta.

Aidha   Watumishi  watatu ambao wapo kwenye masomo ya muda mrefu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kutoka  Divisheni za  Mikataba na Uratibu hawakuzingatiwa katika mgao huo kwa wakati huu kwa kuwa  wapo masomoni.

Menejimenti  imepitisha mgao huo  kwa  Divisheni   na  Vitengo pamoja na majina ya watumishi watakaopatiwa  vifaa hivyo kama ifuatavyo;

1.Divisheni ya  Utawala  watumishi  wanne ( Laptop 4),

2. Divisheni  ya Mikataba  watumishi  25( Laptop 25),

3.Divisheni ya  Uandishi wa Sheria  Watumishi 26 ( laptop 26),

4.Divisheni ya  Uratibu na  Ushauri wa kisheria watumishi 21 ( Laptop 21),

5.Divisheni ya  Mipango  watumishi  wawili ( laptop 2),

5.Kitengo  cha Uhasibu Watumishi wawili ( Laptop2),

6.Kitengo cha Ukaguzi wa  Ndani watumishi 2(laptop 2),

7.Kitengo cha Tehama  watumishi wanne ( Laptop4)

Vile  vile  Menejimenti  ilipitisha mgao wa kumpyuta za Mezani tatu (3) kwa   Divisheni  ya Mikataba(1), Uratibu (1) na Utawala (Dar) 1.

Aidha  Printer cum Scanner ziligawiwa kwa DCT 1,CPD 1  na Masjala ya siri1.  Pia   CPD wamepewa Heavy Duty Printer 1.

Maelekezo ya  Menejimenti ni kwamba  kwa watumishi waliopo  mikoani  na ambao    ni ajira mpya  utaratibu utafanyika  wa kuwafikishia  vifaa hivyo. Jumla ya  Mawakili  wa Serikali  wapya 39 watakuwa  wamepatiwa vitendea kazi  hivyo kwa  mgawanyo wa CPD 10, DCAS15 na DCT 14.

Pamoja na waajiriwa hao wapya kutoka  Divisheni hizo kupatiwa vitenda kazi,  Menejimenti ilielezwa  kwamba bado kutakuwa na upungufu wa vitenda kazi hivyo  kwa Mawakili  16 kutoka  DCAS na DCT ambao watafikiriwa katika awamu  inayokuja.

Aidha  kwa Mujibu  wa Mwenyekiti kwa upande wa  CPD ambao wanafanya zoezi  la urekebu   baada ya  mgao huu Waadishi wa  Sheria  wote  watakuwa  na kumpyuta mpakato.

Aidha  kila   Mkuu wa  Divisheni  na  Kitengo ameelekezwa kusimamia zoezi la ugawaji wa  vifa  hivyo   kuanzia leo Ijumaa  kwa watumishi ambao wapo chini yao kwa kuwasainisha kila mmoja anayekabidhiwa  kifaa hicho

Vile vile  menejimenti  imesisitiza  umuhimu   kwa watumishi wote  wa kuwa na matumizi  sahihi ya vifaa hivyo  hasa katika  kipindi hiki ambacho Taasisi  inatekeleza  majukumu yake  kupitia  mifumo ya Taarifa wa Kielektroniki wa  Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ( OAG-MIS) pamoa na Mfumo wa Mawasiliano ya Serikali  Mtandao (e-Office)   Aidha  suala la utunzaji na uhifadhi salama wa vifaa hivyo limesisitizwa kwa kila mtumishi.

Ikumbukwe pia kwamba  upatikanaji  wa vifaa vya Kisasa vya TEHAMA kwaajili ya  watumishi  na Ofisi  kwa ujumla   umetokana na  kwa kiasi  kikubwa   Juhudi na jitihada za  kubwa  zinazofanywa na Mkuu wa Taasisi  yetu Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Feleshi.

Imeandaliwa na  Kitengo  cha Mawasiliano

26/5/2023