SERIKALI YAWASILISHA MUSWADA WA MAREKBISHO YA SHERIA MBALIMBALI

SERIKALI YAWASILISHA MUSWADA WA MAREKBISHO YA SHERIA MBALIMBALI
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi amewasilisha Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali ya mwaka 2023 ( The Written Laws ( Miscellaneous Amendments) Bill, 2023.
Akiwasilisha Muswada huyo Mwanasheria Mkuu wa Serikali amelieza Bunge kuwa Muswada kama ulivyowasilishwa unapendekeza marekebisho katika Sheria Nane (8)
Akazitaja sheria hizo kuwa ni Sheria ya Usajili wa Wabunifu wa majengo na Wakadiriaji Majenzi sura ya 269 (Architects and Quantity Surveyors ( The Registration) Act,Cap.269; Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229 ( The Media Services Act,Cap.229); Sheria ya Bohari ya Dawa, Sura ya 70 ( The Medical Stores Departiment Act, Cap.70) na Sheria ya Mazishi ya Viongozi wa Kitaifa, Sura ya 419 ( The National Leaders Funeral Act., Cap.419).
Sheria nyingine zilizomo katika Muswada huo ni Sheria ya Reli, Sura ya 170 ( The Railways Act, Cap.170); Sheria ya Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania, Sura ya 277( The Tanzania Forestry Research Institute Act, Cap.277). Sheria ya Mamlaka na majukumu ya Msajili wa Hazina, Sura ya 370 ( The Treasury Registar ( Powers and Functions) Act, Cap 370); na Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani, Sura ya 148 ( The Value Added Tax Act, Cap 148)
Akielezea kuhusu sheria ya mazishi ya Viongozi wa Kitaifa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesema “ sehemu ya Tano ya Muswada inapendekeza marekebisho kwenye Sheria ya Mazishi ya Viongozi wa Kitaifa, Sura ya 419 ambapo kifungu cha 6 kinapendekezwa kufutwa na kuandikwa upya kwa lengo la kuboresha masharti kuhusu mamlaka ya Rais kutoa tangazo la kifo cha kiongozi au kiongozi mahsusi aliye madarakani”
Akasema, marekebishyo hayo pia yanampa mamlaka kiongozi mahsusi aliye madarakani kutoa tangazo la kifo cha kiongozi mahsusi mstaafu.
Dkt. Feleshi amelieleza Bunge zaidi kwamba, marekebisho ya sheria hiyo yanakusudia kutoa mamlaka kwa Rais kutangaza tarehe ya maziko ya Rais aliyefariki akiwa madarakani kuwa ni siku ya mapumziko.
Akasema, lengo la mapendekezo haya ni kuweka bayana na kutofautisha mamlaka zinazopaswa kutoa matangazo ya vifo vya viongozi wa kitaifa na viongozi mahsusi.
Aidha, Mwanasheria Mkuu amebainisha kwamba, Vifungu vya 9 na 10 vinapendekezwa kurekebishwa ili kutoa mamlaka kwa kiongozi mahsusi aliye madarakani kutoa tangazo la kifo cha kiongozi mahsusi mstaafu.
“Lengo la marekebisho haya ni kutambua utaratibu unaotumika sasa ambapo pamoja na kwamba Sheria imemtaja Rais kama mamlaka ya kutoa tangazo la kifo cha kiongozi mahsusi mstaafu, matangazo ya aina hiyo kwa kawaida yamekuwa yakitolewa na viongozi mahsusi walio madarakani”.
Pamoja na maelezo ya ufafanuzi sheria hizo na sheria nyingine zilizowasilishwa katika Muswada huo. Mwanasheria Mkuu wa Serikali alilieleza Bunge kwamba, kwa mujibu wa kanuni ya 99 ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Mwaka 2023, anaomba kutoa hoja kwamba Muswada wa Sheria ya Marekebishyo ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2023 ( the Written Laws ( Miscellaneous Amendments) Bill, 2023 ) kama ilivyorekebishwa kwa mujibu wa Jedwali la Marekebisho ujadiliwe na kupitishwa katika hatua ya Kusomwa kwa Mara ya Pili na ya tatu na hatimaye marekebisho yanayopendekezwa yawe sehemu ya Sheria za Nchi