OMMS YAASWA KUZINGATIA VIASHIRIA HATARISHI KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAKE

Imewekwa: 27 Oct, 2023
OMMS YAASWA KUZINGATIA  VIASHIRIA HATARISHI KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAKE

Imeelezwa kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  inapashwa kuhakikisha kwamba,  udhibiti wa  viashiria hatarishi  unakuwa  sehemu ya  utekelezaji  wa  majukumu ya  .

Hayo  yameelezwa hivi karibuni  na Bw. Elias Madafu kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe wakati wa mafunzo ya siku mbili ( Octoba 24/25)  ya  kuwajengea uelewa  wa Pamoja Risk Champions   kutoka Divisheni na Vitengo  kuhusu Pamoja na mambo mengine suala zima la maeneo gani yanaweza kuwa hatarishi katika  utekelezaji  wa  majukumu ya kila siku ya OMMS.

Bw. Madafu aliwaeleza washiriki  hao  kwamba , kama  Risk Champions  wanaowajibu wa kuagalia au kubaini ni  viashiria gani  hatarishi ambavyo vinaweza  kutokea wakati wa utekelezaji wa majukumu ya kiofisi na ambavyo  vinaweza kusababisha Ofisi  ikashindwa kutekeleza mipango yake na kufikia malengo iliyojiwekea.

“ Baada ya  kujua viashiria hatarishi, unatafuta namna ya kukabiliana  navyo. Hii  itasaidia Ofisi  kufikia malengo yake na kupunguza gharama ambazo zingetokea ikiwa viashiria hivyo  visingeshughulikiwa mapema” akasisitiza  Bw. Magafu

Na kuongeza. “Ni wajibu  wa kila  mtumishi wa OMMS kuhakikisha anatengeneza mazingira  rafiki   na wezeshi ili  kuifanya Ofisi iendelee kutekeleza  majukumu  yake  kwa ufanisi  na kwa kuzingatia taalama yao  na  weledi

 Kwa mujibu wa Divisheni ya Mipango na ambayo ndiyo iliyoandaa mafunzo  hayo  inaeleza  kuwa mafunzo hayo  yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli Miramonti, Dodoma.  washiriki waelimishwa na kujengewa  uwezo  kuhusu  Mfumo wa Viashiria Hatarishi pamoja na kuangalia Rejesta ya Vihatarishi katika kila  Divisheni na Vitengo vyao na pia   kuboresha nyaraka zilizohuishwa kwenye mafunzo ya awali ya Divisheni ya Mipango.

Divisheni ya  Mipango katika taarifa yake inasema  mafunzo yaliyotolewa kwa Risk Champions hao   ni muendelezo baada ya hatua ya awali iliyohusisha Wataalam wa Divisheni walipojengewa  uelewa wa Pamoja  wa namna ya kuandaa na  kuhuisha nyaraka za Mfumo wa Usimamizi wa viashiria hatarishi (Risk Management Framework) na Rejesta ya Viashiria Hatarishi (Risk Register) ya OMMS.

 

Mwisho

27/10/2023