MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI ATOA ANGALIZO KWA WATUMISHI MATUMIZI YA TEHAMA

Imewekwa: 19 Apr, 2023
MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI ATOA ANGALIZO KWA WATUMISHI  MATUMIZI YA TEHAMA

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI ATOA ANGALIZO KWA WATUMISHI  MATUMIZI YA TEHAMA

 

Na Mwandishi  wetu.

Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi  Ofisi ya Mwanasheria  Mkuu wa  Serikali,  Mhe. Jaji Dkt. Eliezer   Feleshi ameelezea matumaini yake kwamba juhudi za kuwawezesha watumishi wa Ofisi ya  Mwanasheria Mkuu wa  Serikali kuwa  na vitenda kazi vya kutosha  vya TEHAMA utawawezesha kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa  majukumu  yao.

Ameyaeleza hayo wakati akimkaribisha  Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe.  Dkt. Damas Ndumbaro ( Mb) kufungua  Mkutano wa  Baraza la Wafanyakazi la  Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Mkutano huo  ulifanyika  Aprili 18, 2023 katika Ukumbi wa Mikutano wa  Ofisi ya Taifa ya Takwimu Mkoani  Dodoma.

Katika taarifa yake kwa  wajumbe wa Baraza  hilo    kuhusu  namna uongozi wa  OMMS ulivyofanya  juhudi za upatikanaji wa vitenda kazi. Mwenyekiti   Jaji Feleshi alieleza kwamba kwa kushirikiana na  wadau mbalimbali  wa Ofisi  , Ofisi imeweza  katika kipindi cha  mwaka wa fedha 2021/2022 hadi Machi 2023, Ofisi imeweza kupata  komputa mpakato na  vishikwamba 160, komputa za  mezani 23, printa 5 na fotokopi moja.

“Mhe. Mgeni  rasmi  vitendea kazi hivi vimesaidia sana kupunguza upungufu mkubwa wa vitenda kazi uliokuwapo.  Tunaamini  vifaa hivi vitaongeza thamani ya  kazi zetu” akaeleza  Mwanasheria  Mkuu  wa Serikali na Mwenyekiti wa Baraza.

Akabainisha  kwamba juhudi hizo za upatikanaji wa vitenda  kazi ni  juhudi endelevu na lengo  hasa ni kuhakikisha kwamba angalau kila mtumishi  anakuwa na  kitendea kazi kitakachomuwezesha kufanya kazi  kijiditali.

Akasema “ tumeshatoa maelekezo ya ndani kwamba  ifikapo Julai Mosi 2023   Ofisi yetu itakuwa kwenye matumizi ya   Ofisi Mtandao ( e-Office) kwa asilimia  mia moja pamoja na  operesheni nyingine”.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali  akatoa rai  na angalizo kuhusu matumizi  ya  Tehama au kufanya kazi  kijiditali.

 Pale aliposema .“Kuhusu matumizi ya  tehama kama nilivyoeleza, jitihada za kupata vitendea kazi hivi  ilikuwa  walau kuiwezesha Ofisi kuweka mazingira bora kwa kila mtumishi  kwamba, anafanya kazi zake kijiditali kwa hiyo  Ofisi kwa  sasa imetimiza wajibu wake wa kuwapatia watendaji vitenda kazi  kwa zaidi ya asilimia 90”. Akasema

Na kuongeza  “tulipokutana  kwenye Baraza la  Mwaka  jana (2022) Mawakili  wetu  wa Mikoa   hawakuwa na  vishikwambi wala kumputa mpakato   kwa sasa wote wanakumputa Mpakato”

Na  katika kuhakikisha kwamba kila mtumishi  anauwezo na maarifa  ya kutumia  vifaa hivyo vya TEHAMA, Mwenyekiti wa Baraza Dk.t Feleshi  aliwaeleza wajumbe wa Baraza  kwamba Ofisi imekamilisha tathimini  ya ndani na akatumia nafasi hiyo  kukipongeza  Kitengo cha TEHAMA cha Mwanasheria Mkuu  wa Serikali  kwa kukamilisha  zoezi hilo  la tathimini zoezi ambalo limebaini kwamba ni watumishi wanne tu ambao  hawana  maarifa ya kutosha ya kutumia  vifaa vya TEHAMA.

Akasisitiza  tena  kwa  kusema. “Kwa hiyo  Wajumbe wa Baraza  eneo hilo  la matumizi ya TEHAMA na kutekeleza majukumu yetu kijiditali ni moja wapo  ya eneo  nililosema ikifika  Julai Mosi 2023 litatosha  kumuondoa  Mtumishi kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali”.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali  akatumia fursa hiyo kuwashukuru wadau wote ambao wamesaidia na wanaendelea kuisaidia vitendea kazi Ofisi ya Mwanasheria  Mkuu wa Serikali  huku akitoa  shukrani  za pekee  kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.