MIKATABA ITAPELEKWA BUNGENI KWA MUJIBU WA MATAKWA YA KISHERIA-AG FELESHI

Imewekwa: 13 May, 2022
MIKATABA ITAPELEKWA BUNGENI KWA MUJIBU WA MATAKWA YA KISHERIA-AG FELESHI

MIKATABA ITAPELEKWA BUNGENI KWA MUJIBU WA MATAKWA YA KISHERIA-AG FELESHI

Na Mwandishi wetu

Dodoma

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji  Dkt. Eliezer Feleshi amelihakikishia   Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba,  Mikataba ile ambayo inatakiwa  kuridhiwa na Bunge  itapelekwa katika chombo hicho  kwa mujibu wa  matakwa ya kisheria.

Ameyasema hayo  hivi karibuni  wakati alipokuwa akichangia na kujibu  michango iliyotolewa na wabunge  baada ya  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndubaro ( Mb).     Bajeti ya  Wizara ya  Katiba na  Sheria  na Taasisi zake katika Bunge la  12, Mkutano wa 7 wa Bunge la bajeti, Kikao cha 14.

“Mhe. Spika,  ninao wajibu mahususi wa mambo yanayohusu mikataba, wajibu wa kwanza, ni kwa ile mikataba inayotakiwa kuridhiwa na Bunge hili, kwa mujibu wa Ibara ya 63 Ibara ndogo ya 3 (e). Ofisi yangu itaendelea kuhakikisha Mikataba  inayotakiwa kuletwa na kuridhiwa na bunge inaletwa kwa kufuata matakwa ya Katiba na  sheria zetu”

Akitolea ufafanuzi  zaidi   kuhusu suala hilo la  mikataba na  ambalo liliibuliwa  na baadhi ya wabunge, AG Feleshi ameliambia  Bunge hilo. “ Tunapoongelea masuala ya mikataba,  mikataba yote inayofuata sheria inaoongozwa na sheria na kwa ushiriki wa Bunge hilo.

Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali,  amesema, katika utekelezaji wa wajibu  huo wa kuwasilisha Mikataba  bungeni,  hajaona kama kuna lalamiko la mikataba inayotakiwa kuletwa bungeni haijaletwa.

Akawakumbusha wabunge kwamba, wanaowajibu  wa kuisimamia Serikali   kupitia Kamati za Bunge hilo  tukufu  kamati ambazo zinasimamia Wizara  na kila Taasisi ya Serikali.

Kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu, Kamati hizo zina wajibu  pamoja na mambo mengine, wajibu  wa kutembelea miradi kule ilipo ambako kazi zinaendelea. “Na kazi hiyo ni pamoja  na kujua takwa la mikataba ya miradi hiyo. Kwa hiyo  niamini kwamba Bunge hili  na kamati zake litaendelea kuhakikisha zile  Kamati zinapewa fursa za kuwianishia miradi iliyopo  na mikataba husika”

Aidha amesema, kwa zile Kamati za Bunge zinazosimamzia utendaji wa Serikali,  kuliko  na mikataba hiyo , zimenyimwa fursa ya kujua mikataba  hiyo ina nini, ukiacha mikataba  inayoletwa hapa Bungeni , basi   serikali  ipo  tayari +kupokea hoja kama kuna ukiukwaji huo na kushughulikia.