MENEJIMENTI YAKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA JENGO JIPYA LA OMMS

Imewekwa: 21 May, 2022
MENEJIMENTI YAKAGUA   MAENDELEO YA UJENZI WA JENGO  JIPYA LA  OMMS

Na  Mwandishi wetu

Mji wa Serikali, Mtumba

Menejimenti ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  ikiongozwa na  Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Evaristo  Longopa

Mei 16  walitembelea , kukagua na kujionea  maendeleo ya ujenzi wa Jengo jipya la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Jengo hilo  lenye umbo la herufi Y   litakalo kuwa na   gorofa tano  linajengwa mkabala  ya Ofisi za sasa za OMMS zilizopo katika  Mji wa Serikali  -Mtumba Jijini Dodoma.

Timu ya  Menejimenti  ilipatiwa  maelezo ya  hali ya  ujenzi ambapo  Mhandisi  Evans Mwingizi alieleza kwamba licha ya  jengo  hilo kuwa na mwonekano  tofauti na  majengo mengine ya wizara mbalimbali   yanayoendelea kujengwa  katika Mji huu wa Serikali,  Jengo la  OMMS  litakuwa  jengo kubwa na   lenye majengo  matano kwa pamoja.

Akizungumzia kuhusu   ujezi Mhandisi Mwingizi  alisema kazi inakwenda  vizuri  licha ya changamoto mbalimbali walizopata wakati wa kipindi cha mvua na   mabadiliko ya mchoro kwa kuongeza  Lift , kwa sasa kazi inaendelea vizuri.

Kwa upande wao Mejejimeti ilielezea kuridhishwa kwake na mwenendo mzima wa ujenzi wa Jengo hilo jipya

Jengo hilo   linajengwa na kampuni ya Ujenzi ya SUMA JKT. Mradi mzima utagharimu shilingi  Bilioni 28.6

Ujenzi huo  unatarajia kuchukua miezi 24.