MAJALIWA AISHAURI OMMS KUSHUKA KWA WANANCHI

Imewekwa: 27 Apr, 2023
MAJALIWA AISHAURI OMMS KUSHUKA KWA WANANCHI

MAJALIWA AISHAURI OMMS KUSHUKA KWA WANANCHI

Na  Mwandishi  Wetu

27/4/2023

Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa  ameishauri Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  kuweka mifumo  ya kuwafikia wananchi  waliowengi  wanaohitaji  Msaada wa Kisheria.

Ametoa ushauri huo leo  ( Alhamisi) wakati alipotembelea  Banda la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  muda mfupi kabla ya  uzinduzi wa  Kampeni ya Msaada wa Kisheria ( Mama Samia Legal Aid Campaig), uzinduzi  uliofanyika katika   Ukumbi wa Chimwaga- Chuo Kikuu cha Dodoma. 

Akiwa  katika  Banda   hilo la  OMMS,  Mkurugenzi Msaidizi Ushauri wa Kisheria Harroun  Matagane Pamoja na  mambo mengine alimuelezea Mhe. Waziri Mkuu namna ambavyo  Ofisi  imekuwa ikipokea  maombi ya  msaada wa  wa  ushauri wa  kisheria.

” Mhe  Waziri  Mkuu  pamoja na ushauri   wa kisheria tunaoutoa kwa Wizara na Taasisi za Serikali na Wadau wengine,   pia  tunapokea maombi  kutoka kwa wananchi wanaoomba ushauri au msaada wa kisheria katika  maeneo mbalimbali ,  kwa mafano katika  kipindi cha  Julai, 2022 hadi  March   2023  maombi ya ushauri wa kisheria 812  yalipokelewa na kufanyiwa  kazi. Kati  ya maombi hayo 812, 149 yalitoka kwa wananchi” . Akaeleza  Mkurugenzi Msaidizi  Harroun Matagane

Baada ya   taarifa hiyo,  ndipo Waziri Mkuu   Kassim Majaliwa alipotaka kufahamu kwa kina  kama   Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  inao mfumo   unaofika  mpaka katika  halmashauri ambako amesema  ndiko  waliko wananchi wengi.

Akasema  ingependeza au ingefaa  endapo  Ofisi itaangalia   uwezekano  wa kuwa na mfumo huo wakuwafikia wananchi waliowengi wenye shinda za kisheria badala ya  kuishia katika ngani  ya mikoa tu.

Pamoja na ushauri huo Waziri Mkuu  Majaliwa  ametumia  fursa hiyo kuipongeza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  kwa utekelezaji  mzuri wa   Majukumu yake. “ Ninatambua  utekelezaji  mzuri wa majukumu  yenu na katika hili  ninawapongeza sana”.

Aidha Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro alitoa ufafanuzi  wa kwanini OMMS haijafika mpaka ngazi ya Wilaya akisema Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali inashirikiana kwa  karibu na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali  .

  Akizungumza  kabla ya  kumkaribisha  Waziri Mkuu  kuzindua kampeni hiyo,  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas  Ndumbaro ( Mb) alisema   utekelezaji wa kampeni hiyo unatokana na  ridhio la Mhe. Samia Suluhu  Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania  ambaye wakati wa Mkutano Mkuu wa Mawakili  wa Serikali  uliofanyika  Septemba 29,2022 Mkoani Dodoma aliridhia jina lake kutumika katika Kampeni hiyo.

Akizungumzia Zaidi   kuhusu  utekelezaji  wa kampeni hiyo,   Waziri Ndumbaro amesema Wizara itashirikiana na  Wizara na Taasisi  mbaliambli za Serikali  na  Wadau wengine wa ndani na  nje.

Baadhi ya  Taasisi za Serikali ambazo Mhe. Waziri  alisema  zitashiriki katika zoezi hilo ni Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Aidha   baada  ya uzinduzi  uliofanyika  leo    huduma za ushauri na msaada wa kisheria  zitaanza kutolewa  katika Wilaya  zote za Mkoa wa Dodoma na  Halmashauri zake  viwamo  baadhi ya vituo vya polisi na magereza  zoezi litakalokwenda hadi  tarehe 7/5/2023. Kwa mkoa wa Dodoma

Akasema baada ya  mkoa wa Dodoma,  Mikoa itakayofuatia ni  Shinyanga,  Manyara  na Ruvuma na ratiba kwa  mikoa mingine  itatangazwa  baadaye. Aidha  kampeni hii itafanyika pia   Visiwani  Zanzibar  na Pemba.

Akizindua  Kampeni Mama  Samia Legal Aid Campaign  ni mpango wa miaka mitatu.

Kwa upande wake  Mhe. Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa akizindua Kampeni hiyo ametoa wito kwa wananchi wanaohitaji  ushauri na msaada wa kisheria  kuitumia fursa hii na hasa kwa kuwa ni  bure na itawafikia  wananchi pale walipo.

Akawataka  viongozi wote katika ngazi mbalimbali  wakiwamo  wa Taasisi za Dini kutoa ushirikiano  ikiwa ni Pamoja na  kutoa taarifa  zinazohusu matukio ya kikatili yanayofanyika katika maeneo yao husani wanawake, Watoto na makundi mengine yaliyokatika  mazingira  magumu.

Aidha amewataka na kuwahimiza viongozi  hao  kutoa taarifa za  uwepo    mambo yasiyozingatia maadili na utamaduni na mila za kitanzania   katika maeneo yao na pia kutowafisha watuhumiwa.

Kauli mbiu ya Kampeni hii  ni  “Msaada Wa Kisheria Kwa Haki, Usawa Amani na Maendeleo”

Imeandaliwa na  Kitengo cha Mawasiliano