BUNGE LAPITISHA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

Imewekwa: 25 Apr, 2023
BUNGE LAPITISHA  BAJETI YA  WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

 YALIYOJILI KWA UFUPI WASILISHO  LA  BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

Na Mwandishi wetu

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  katika  Mkutano wake wa Kumi na Moja , Kikao  cha   kumi na  Tano  kilichoketi   leo  jumanne (Aprili 25/2023) limepitisha  Bajeti ya  Wizara ya Katiba na Sheria.

Katika  kikao hicho  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas  Ndumbaro (Mb) aliliomba   Bunge kuidhinisha jumla ya Shilingi Bn 383,619,511,000   kwaajili ya  matumizi ya kawaida  na miradi ya  maendeleo.

Kiasi hicho cha fesha kiliombwa na kupitishwa na  Bunge ni  kwaajili ya Wizara na Taasisi  zake   Nane (8).Mafungu hayo ni  Fungu 12 ambalo ni  la Tume ya Utumishi wa Mahakama, Fungu 16 Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali , Fungu 19 Ofisi ya Wakili  Mkuu wa Serikali na Fungu 35 Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

Mafungu mengine ni  Fungu 40 Mfuko wa Mahakama,  Fungu 41 Wizara ya Katiba na Sheria ( RITA/LST) Fungu 55 Tume ya Haki za Binadamu na Utawala  Bora  na   Fungu 59 Tume ya Kurekebisha Sheria.

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Fungu 16  imetengewa  kiasi cha Bn 18,817,867,000.00 kwa mchanganuo  ufuatano

Matumizi ya Misharaha  ni  Bn 4,072,737,000.00

Matumizi ya  Mengineyo Bn 12,290,130,000.00

Matumizi mengineyo ( Ndani) Bn2,000,000,00.

Matumizi mengineyo ( Nje) sh 455,000,000.00

Aidha Mwanasheria Mkuu wa Serikali   Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki  Feleshi  alijibu na kutoa ufafanuzi  wa hoja mbalimbali  zilizowasilishwa  na Waheshimiwa Wabunge

Hotuba ya Bajeti inapatikana  katika  Wavuti ya  Ofisi