AG FELESHI AKUTANA NA WATAALAMU WA BSAAT

Imewekwa: 08 Dec, 2022
AG FELESHI  AKUTANA NA  WATAALAMU WA  BSAAT

Na Mwandishi  Wetu

Dodoma

8/12/2022

Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Feleshi leo  (Alhamisi) amekutana na  kufanya  mazungumzo na   timu ya wataalamu  inayofanya tathmini ya utekelezaji wa  Mradi  wa Mapambano  Endelevu dhidi ya Rushwa Tanzania (BSAAT).

Mazungumzo  kati ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na timu hiyo  inayoundwa na  Wataalamu kutoka  Nchini  Uingereza wakishirikiana na FCDO  Pamoja na  waratibu wa mradi huo kutoka Ofisi ya Rais Ikulu   yamefanyika katika Ukumbi wa Mkutano wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Mtumba Jijini Dodoma.

Akitambulisha  wataalamu  hao, Mratibu wa BSAAT Dkt. Bonaventura Baya  alimueleza Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwamba,  wataalamu  hao  wapo katika ziara ya    kutathimini utekelezaji wa mradi wa mapambano  endelevu dhidi ya Rushwa Tanzania ili  kubaini  mafanikio na changamoto.

 Akabinisha kuwa imekuwa  heshma kubwa  kwa timu hiyo  kupata fursa ya  kukutana na kufanya  mazungumzo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali  pamoja na wataalamu wake.

Katika  mazungumzo hayo na ambayo yalichukua zaidi ya saa moja, Mwanasheria Mkuu wa Serikali   Dkt. Feleshi  pamoja na kuwasilisha  tathmini yake na ushiriki wa Ofisi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika mradi huo,  pia ameishukuru  Timu  hiyo ya Wataalamu  kwa  kumtembelea Ofisini kwake lakini pia kupata fursa ya kukaa ana kwa ana  na wataalamu hao na kubalishana  mawazo  kuhusu mafaniko na changamoto  katika utekelezaji wa  Mradi huo.

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  ilianza  utekelezaji wa programu mbalimbali za BSAAT mwezi April mwaka huu kwa kuwa na vikao kazi vilivyofanyika katika Mikoa ya Mwanza, Iringa na Arusha.

Aidha baada ya  vikao kazi hiyvo shughuli  mbalimbali zimekuwa zikiendelea  chini ya  ufadhili wa  BSAAT.

Katika mazungumzo hayo Mwanasheria Mkuu wa Serikali  aliambatana na  Bi. Ndeonika Mwaikambo  ambaye ni Mratibu wa Mradi huo katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa  Serikali, Bi. Upendo Ndosi ( Mchumi) Bw. Meja Kulaya ( Mhasibu) na  Bw.  Fredy  Nyaroga  na Christopher  Bwire ( IT)

 Mradi wa Mapambano  Endelevu dhidi ya Rushwa  Tanzania ( BSAAT) unaratibiwa na Ofisi ya Rais  Ikulu  kwa ufadhili wa  Serikali ya Uingereza na  Jumuiya ya Ulaya